Overview

Asili ya Parokia ya Theresia wa Mtoto Yesu ni Parokia ya Mt. Peter Claver na Theresia wa Mtoto Yesu ya Mbezi Luis. (Parokia hii ilikuwa inasimamiwa na watakatifu wawili). Eneo hili lilinunuliwa na Parokia hii mwaka 2002/3. Awali lilikuwa ni shamba lililomilikiwa na muumini mmoja aliyeitwa Bwana Kaduri ambaye alipenda kuliuza kwa kanisa. Gharama za kukunua shamba hili ilitokana kwa kiasi kikubwa na michango ya waamini. Parokia ya Mt. Peter Claver/Theresia wa Mtoto Yesu ililinunua kwa lengo la kuhamishia Parokia eneo hilo kwa vile eneo kubwa la Parokia ya Mbezi Luis likiwemo kanisa lenyewe na nyumba ya mapadri lilikuwa kwenye eneo la hifadhi ya Barabara.

Client:Parokia ya Mt. Theresia Wa Mtoto Yesu Mbezi-Mwisho
Link: https://parokia-theresia.or.tz/